Takwimu kuhusu utafiti wa UNICEF OGIP

Nchi Zinazoshiriki
55
Jumla ya Wajibu
80,189

Tovuti ndogo ya shirika la UNICEF na mfululizo wa ripoti

Kuhusu Mradi wa Utoto Unaobadilika

Motisha

Tunaishi katika enzi ya mabadiliko ya haraka na makubwa. Kadiri ulimwengu unavyobadilika — kuwa wa kidijitali zaidi, wenye utandawazi zaidi, na anuwai zaidi — utoto unabadilika nao. Mradi wa Utoto Unaobadilika — ushirikiano kati ya UNICEF na Gallub — uliundwa ili kuchunguza mabadiliko haya, na kuelewa vyema zaidi inachomaanisha kuwa mtoto katika Karne ya 21. Mradi huu unanuia kujibu maswali mawili: Kukua leo kuko vipi? Na vijana wanaona ulimwengu kwa utofauti kwa njia ipi? Ili kujibu maswali haya, tulitaka kusikia kutoka kwa watoto na vijana wenyewe. Kulinganisha uzoefu na mitazamo ya vijana dhidi ya watu wenye umri mkubwa hutoa mwelekeo thabiti wa kuchunguza jinsi utoto unavyobadilika, na mahali ambapo vizazi hutofautiana na kuungana. Lengo kuu la mradi ni kuwafanya vijana kuwa sehemu muhimu— uzoefu wao na matarajio — katika kazi ya kuboresha maisha ya watoto wote, leo na katika siku zijazo.

Tovuti ndogo

Tovuti hii ndogo ilitolewa na UNICEF ili kuwawezesha watu kutoka duniani kote, hasa watoto na vijana, kuangazia maswali ya Mradi na kuchunguza matokeo yake. Tunatumai itakufurahisa! Tovuti hii ndogo ilitengenezwa na kampuni ya kusanifu, CLEVER°FRANKE. Hakuna data kuhusu watumiaji inayokusanywa kupitia kwa tovuti hii ndogo.

Matokeo yanayoonyeshwa kwenye tovuti hii ndogo yanatokana moja kwa moja na data ya utafiti iliyobainishwa hapa chini. Marejeleo ya "vijana" inarejelea kikundi cha watu wenye umri mdogo zaidi katika tafiti zote mbili: watu wenye umri wa miaka 15 hadi 24. Marejeleo yote ya idadi ya jumla au ya wastani — k.m., “kwa wastani” au “wastani wa”— inarejelea matokeo ya utafiti ya swali mahususi la nchi ya wastani katika nchi zote zilizojumuishwa katika utafiti. Pia, “wastani” wa kikundi cha mapato cha nchi mahususi umetolewa kwenye matokeo ya utafiti kutoka kwa nchi ya wastani kwenye kikundi hicho.

Tafiti

Ili kuchanganua maswali na mada za Mradi, shirika la UNICEF na shirika la Gallup yameshirikiana kwa tafiti mbili za kimataifa za rika nyingi.

Mihtasari iliyobainishwa kuwa “MPYA” inaonyesha data iliyotolewa kwenye kazi ya shirika la UNICEF na mradi wa hivi karibuni zaidi wa Gallup World Poll. Mingine yote inatokana na data iliyotolewa kwenye utafiti wa UNICEF-Gallup wa 2021.

Utafiti wa UNICEF-Gallup wa 2021

Kwa awamu ya kwanza ya Mradi wa Changing Childhood, shirika la UNICEF na shirika la Gallup yaliunda utafiti maalum ulioendeshwa katika nchi 21 duniani. Kwa kutumia utaalamu wake unaotokana na kuendesha mradi wake wa kila mwaka wa World Poll, shirika la Gallup lilifanya utafiti kwa sampuli wakilishi za angalau watu 1,000 katika kila nchi (1,500 nchini India). Katika kila nchi, sampuli iligawanywa katika makundi mawili ya umri: watu wenye umri wa miaka 15 hadi 24 (kulingana na ufafanuzi wa Umoja wa Mataifa wa neno kijana), na watu wenye umri wa miaka 40 na zaidi. Tafiti zilifanyika kati ya mwezi wa Februari na Juni 2021. Washiriki wote walishiriki kupitia simu. Kwa kubuniwa kwa msaada wa wataalamu mbalimbali, zana za utafiti ni pamoja na maswali yaliyokuwa yameulizwa katika kura nyingine, pamoja na maswali mapya yaliyobuniwa hasa kwa Mradi wa Changing Childhood.

Kulingana na ukubwa wa sampuli za nchi, na ugawanyaji wa sampuli katika makundi mawili ya rika, matokeo mengi yaliyotokana na data ya utafiti huu yana tofauti ya hitilafu ya karibu alama +/- 4 za asilimia katika uaminifu wa kiwango cha asilimia 95. Tofauti za hitilafu zitakuwa kubwa kwa vikundi vidogo vya watu. Maelezo zaidi kuhusu jinsi ya kufafanua matokeo yanapatikana kwenye ukurasa wa mbinu iliyotumika hapa.

UNICEF + Gallup World Poll

Kwa awamu ya pili ya Mradi wa Changing Childhood, shirika la UNICEF lilishirikiana na shirika la Gallup katika mradi wake wa hivi karibu zaidi wa World Poll. Tulirejesha maswali matano ya maswali 32 ya kwanza ya Mradi wa Changing Childhood nyanjani katika mwaka wa 2022-2023 – wakati huu katika nchi 55 (nchi 21 za kwanza pamoja na nchi 34 za ziada). Maswali yanazingatia sehemu nne: changamoto ya hali ya anga, vyanzo vya habari, uaminifu na utambulisho. Sampuli zote zinategemea welekeo na uwakilishi wa kitaifa, kwa kutumia ukubwa wa sampuli wa karibu watu 1,000 wa umri wa miaka 15 na zaidi katika kila nchi. Eneo linalolengwa ni nchi nzima, ikiwa ni pamoja na mashambani, na ukubwa wa sampuli unawakilisha raia wote, watu ambao hawajasajiliwa kama raia wa nchi.

Kulingana na ukubwa wa sampuli za nchi, matokeo mengi yanayoonyeshwa kwenye tovuti ndogo yana tofauti ya hitilafu ya karibuni alama ±4 za asilimia katika kiwango cha uaminifu cha asilimia 95. Tofauti za hitilafu ni kubwa kwa vikundi vidogo vya watu. Kwa kikundi cha vijana, tofauti ya wastani ya hitilafu kwa kikundi cha watu wenye umri wa miaka 15 hadi 24 katika nchi zote 55 ni asilimia +-/7.6. Kwa maelezo zaidi kuhusu sampuli za utafiti au tofauti za hitilafu, tafadhali angalia muhtasari wa mbinu iliyotumika wa mradi wa Gallup World Poll hapa au wasiliana nasi kupitia anwani ya barua pepe iliyo hapa chini.

Jifunze zaidi

Uchanganuzi wa kina zaidi wa matokeo ya Mradi unapatikana kwenye ripoti za Mradi zilizounganishwa kwenye ukurasa huu. Watumiaji ambao wangependa kupata uchanganuzi zaidi wanahimizwa wasome hojaji, mbinu zilizotumika, data ndogo yote na vitabu vya misimbo – pia vinapatikana kwenye ukurasa huu. Tungependa kusikia utakachogundua kutokana na uchanganuzi wako mwenyewe. Ikiwa una maswali au ungependa kutueleza jinsi unavyotumia Mradi, tafadhali tutumie barua pepe kupitia Changing-Childhood@unicef.org.

Rudi kwa utangulizi