Habari
Je, kusogeza ni kuamini?
Vijana hutumia majukwaa ya mitandao ya jamii zaidi ya watu wenye umri mkubwa. Lakini wanayaamini kwa kiwango kipi?
Tulifanya utafiti miongoni mwa watu wenye umri wa miaka 15-24 na 40+ katika nchi 21 ili kuchunguza jinsi utoto unavyobadilika.
Soma zaidi kuhusu utafitiJibu swali lililo hapa juu ili kujifunza zadi kuhusu hali inayobadilika ya utoto.
Rudi kwenye swaliMajukwaa ya mitandao ya jamii ndiyo njia kubwa zaidi ambayo kwayo vijana hupata habari zao. Hiyo haimaanishi kuwa wanaamini kile wanachosogeza.
Kwa wastani, ni 17% kati ya vijana wanasema wana imani "nyingi" kwa habari kutoka kwa majukwaa ya mitandao ya jamii.
Hili ni fungu dogo ikilinganishwa na wale walio na imani nyingi kwa vyombo vya habari vya zamani vya kitaifa na vyombo vya habari vya kimataifa, madaktari na wafanyakazi wa huduma za afya, na wanasayansi - katika kila chanzo tulichouliza kuhusu!
Huku vijana wakitambua kuwa si kila jambo wanalosoma ni ukweli, kwa jumla wanaripoti kiwango kikubwa cha imani kuliko watu wenye umri mkubwa kwa vyanzo mbalimbali vya habari na taasisi.
Kuna chombo kimoja tu ambacho vijana wanaripoti kiwango kidogo cha imani kwake kuliko watu wenye umri mkubwa:
Taasisi za kidini
Kwa kulinganisha, vijana wanaripoti viwango vikubwa vya imani kuliko watu wenye umri mkubwa katika vyanzo vifuatavyo vya habari:
Majukwaa ya mitandao ya jamii
Serikali ya kitaifa
Vyombo vya habari vya kimataifa
Wanasayansi
Huku vijana kwa wastani wakionyesha imani kubwa kiasi kwa mitandao ya jamii kuliko watu wenye umri mkubwa, kuna ukinzani katika hadithi hii:
Miongoni mwa watu wanaotegemea mitandao ya jamii ili kupata habari zao, 24% kati ya vijana wana uwezekano mdogo wa kuripoti imani nyingi kwa majukwaa ya mitandao ya jamii ikilinganishwa na watumiaji wenye umri mkubwa.
Imebainika kuwa idadi kubwa ya vijana wanaotumia mtandao kote duniani ni watumiaji wanaotambua wanachosoma mtandaoni.